Kutambua mchango wako kwenye yote unayopitia.

Kwenye maisha ni rahisi sana kulalamika na kuwalaumu wengine pale tunapokutana na matatizo au changamoto fulani kwenye maisha.

Labda watu wamekudanganya, wamekuibia, wamekusaliti au kukutelekeza. Ni rahisi kulaumu wengine na kufarijika na lawama hizo. Ila haitakuwa na msaada wowote kwako.

Njia bora ya kukabiliana na hali ya kulalamika na kulaumu ni kuchukulia kila kitu ni makosa yako. Hata kama mtu kakudanganya, ni wewe umempa nafasi mpaka akakudanganya, ni wewe mwenyewe umemwamini.

Kuchukulia kila kitu ni makosa yako ni bora kuliko hata kusamehe. Maana unaposamehe bado unakuwa unaamini Uliyemsamehe ndiye mwenye makosa. Lakini unapokubali kila kitu ni makosa yako, unajiondoa kwenye hali ya mambo fulani kujirudia rudia kwako.

Hili linakupa nguvu kubwa ya kuona kila kitu ni wajibu wako hivyo utachukua hatua sahihi na kuweza kujiboresha mwenyewe.

Imeandikwa na mwandishi na mshauri.

Maureen Kemei.

Blog, kufikirichanya.wordpress.com.

By Maureen Kemei

Author, psychologist.

Leave a comment

Your email address will not be published. Required fields are marked *