Karibu, hakuna wakati binadamu atasema amekamilika kwa namna yoyote ile, au kwa vile anavyotaka. Hakuna wakati ambao dunia itakuwa Sawa na kila unachohitaji kitakuwa kimekamilika kama unavyotaka.
Kusubiri hadi kila kitu kiwe Sawa ni kujichelewesha. Unachohitaji ni kuwa na kusudi, kuwa na nia njema ya kufanya na kisha kufuata mchakato sahihi.
Kibaya zaidi ni pale tunaposahau kusudi letu hapa duniani na kuanza kujishughukisha na mambo yasiyokuwa na tija yoyote katika maisha.
Kusuluhisha hali hili la kusahau kusudi la maisha ni kukaa kwenye mchakato sahihi, huku ukisukumwa na nia njema na fursa nzuri zaidi inafunguka enyewe.
Hata pale unapoona hakuna njia kabisa, usikate tamaa au kujizuia, badala yake songa mbele na nia yako na fuata mchakato sahihi, njia zitafunguka na utaweza kusonga mbele zaidi.
Chukua hatua, amua kuwa na kusudi la maisha, alafu ufuate mchakato sahihi, ukiendeshwa na nia njema na kwa kweli utafanya makubwa.
Asante, akujaliye sana.
Maureen Kemei.
Blog, kufikirichanya.wordpress.com
Email, kemeimaureen7@gmail.com