Rafiki yangu mpendwa, sina uhakika kama itakufaa, lakini Robin ila Ro anatushirikisha hadithi ya Niki lauda, mshiriki wa mbio za magari ambaye alipata ajali mbaya kwenye mashindano na kuungua kichwa na uso.
Alipelekwa hospitalini akiwa taabani na kila mtu alijua hawezi kupona. Lakini siku 40 baadaye alirudi kwenye mbio za magari, kabla hata hajapona vizuri.
Alipoulizwa alieleza kilichomwezesha kupona ni alikataza akili yake kupumzika, kwani alijua kwa hali aliyokuwa nayo, angeruhusu akili ipumzike kingekuwa kifo.
Na pia alieleza baada ya kuona amepata nafuu, alichagua kurudi kwenye mbio za magari kwa sababu ndiyo kitu muhimu zaidi kwake.
Kupitia hadithi hii Robin anatupa mafunzo matatu makubwa.
Kwanza ni kujenga ujasi, hakuna anayezaliwa akiwa jasiri, Bali ujasiri hutengenezwa kadiri mtu anavyokabiliana na magumu. Hivyo unapokutana na magumu, usilalamike wala kuyakimbia, bali yakabili na yatumie kujenga ujasiri.
Mbili ni rudi kwenye mwendo mapema. Unapokutana na magumu ambayo yanakutoa kwenye mwendo, hakikisha unarudi kwenye mwendo mapema iwezekanavyo.
Magumu hayo yanaweza kukujengea hofu ambayo itaendelea kukupa hofu kadiri utakavyokuwa nje ya mwendo kwa kurudi kwenye mwendo mapema, utavunja hofu hiyo na kuimarisha ujasiri wako.
Tatu ni usistaafu. Hata baada ya Niki lauda kustaafu mbio za magari, aliendelea na ujasiriamali kwenye sekta ya usafiri. Licha ya kuwa alikuwa ameshafika kwenye kilele, hakuona huo ndiyo mwisho, aliendelea kujisukuma zaidi.
Hivyo ndivyo alivyopaswa kuwa pia, kutokukubali kustaafu baada ya kufika kileleni, badala yake kuendelea kujisukuma na kufanya makubwa zaidi.
Mwandishi wako,
Maureen Kemei.
kemeimaureen7@gmail.com.