Rafiki yangu mpendwa unapochagua kitu ambacho utakifanya, unapaswa kukifanya kweli hadi kikamilike.
Wengi hushindwa kwenye hili kwa sababu huhadaiwa na fursa nyingi mpya zinazowajia. Wanaacha kile walichochagua kufanya na kuanza kuhangaika na vitu vingine.
Sina uhakika kama itakufaa, lakini kama unataka kufanikiwa usiwe kama hao wengi. Tumia kigezo cha NDIYO KUBWA kuchagua kile muhimu kwako kufanya.
Na ukishasema NDIYO kwenye kitu kimoja, sema HAPANA kwenye vingine vyote mpaka utakapokamilisha hicho kimoja muhimu kabisa.
Chukua hatua; rafiki ni bora tunaposema NDIYO kwa kitu kimoja, tuseme HAPANA kwenye vingine vyote.
Uwe na wakati mwema.
Rafiki na mwandishi wako,
Maureen Kemei .
kemeimaureen7@gmail.com.
uamshobinafsi.com.