Je, Unajua Wewe U Adui Wako M8wenyewe?

Rafiki yangu mpendwa moja ya changamoto kubwa zinazowazuia watu wengi kufuata kile wanachotaka ili kufikia mafanikio wanayotarajia ni kuwa wapinzani wao wenyewe.

Kuwa adui wangu mwenyewe ni kikwazo namba moja kwangu kwenye kubadili maisha yangu na kufikia mafanikio makubwa.

Kama sitaacha kuwa adui wangu mwenyewe hakuna kitakachobadilika maishani mwangu.

Safari ya kuibadili maisha yangu na kufikia mafanikio sio rahisi kama ninavyofikiria , nitapata upinzani mkubwa kuanzia ndani yangu mwenyewe na hata kwa wale wanaonizunguka .

Kama nataka kufaulu kwenye mambo ninayofanya nahitaji kukataa kabisa kuwa mpinzani wangu mwenyewe na kuanza kujikubali na kujitamkia maneno chanya yatakayonisaida kufikia ndoto zangu kubwa.

Najua mara nyingi nimekuwa mpinzani wangu mwenyewe nimekuwa napanga kubadili maisha yangu ili kufikia mafanikio, Lakini mimi mwenyewe naanza kupinga vile nilivyopanga kufanya .

Chukua hatua; kuanzia leo naondoa kabisa upinzani mkubwa ambao nimekuwa najiwekea mwenyewe.

Rafiki na mwandishi wako,

Maureen Kemei.

kemeimaureen7@gmail.com.

By Maureen Kemei

Author, psychologist.

Leave a comment

Your email address will not be published. Required fields are marked *