Rafiki yangu mpendwa sina uhakika kama itakufaa, lakini kuna njia mbili ya kuishi.
Njia ya kwanza ni kuishi kama ambavyo watu wanataka wewe uishi. Kwa kufanya na kuishi kama vile wengine wanataka ni kujichelewesha mwenyewe na pia ni kama kuruhusu wengine waendeshe maisha yako.
Sifanyi kile ambacho kila mtu anafanya hata kama sina msukumo wowote wa kufanya hivyo.
Njia ya pili ni kuishi kama vile ambavyo mimi mwenyewe nataka kuishi. Kufanya kile ambacho ni muhimu kwangu.
Kufanya kazi kwa juhudi na maarifa hili kuweza kufikia ndoto zangu kubwa, bila kujali wengine wanafanya nini au wanasema nini.
Hatua ya kuchukua; najua maisha ni kuchagua, na kuna njia mbili za kuweza kuishi maisha yangu.
Mimi nachagua kuishi njia yangu ya kuishi kama vile nataka na nitafanya mambo ninayopenda hili kuhakikisha maisha yangu yanakwenda vile nilivyopanga.
Mwandishi na rafiki yako,
Maureen Kemei.
kemeimaureen7@gmail.com.
www uamshobinafsi.com.