Umuhimu Wa Kutoa Kafara.

Rafiki, kila mtu kwenye maisha kuna kafara anayotoa, kitu muhimu anachoamua kukipoteza ili kupata kingine anachokihitaji zaidi.

Wanaofanikiwa na kupata utajiri ni wale wanaotoa kafara ya muda. Hawa wanautumia muda mwingi kwenye kazi zao na kukosa muda wa starehe mbalimbali. Hawa huonekana kama hawana mlinganyo wa maisha, lakini huishia kuwa na maisha bora.

Wasiofanikiwa na wanaobaki kwenye umaskini huwa wanatoa kafara ya ndoto zao. Hawa wanakubali kuzika ndoto kubwa walizonazo ili waendelee kuishi maisha ya kawaida. Wanafanya kazi zao kwa muda wa kawaida na baada ya hapo hupumzika na kustarehe. Kinachotokea ni wanakuwa na maisha ya kawaida na ya chini kabisa.

Chukua hatua; rafiki yangu amua leo ni kafara ipi unatoa, kuweka muda wako kwenye kazi na kuachana na starehe na anasa au kuendekeza starehe na anasa na kuzika ndoto yako?

Rafiki chagua kwa usahihi halafu usiwe na malalamiko tena.

Rafiki yako,

Maureen Kemei.

kemeimaureen7@gmail.com.

uamshobinafsi.com.

By Maureen Kemei

Author, psychologist.

Leave a comment

Your email address will not be published. Required fields are marked *