Rafiki yangu mpendwa kanuni hii huwa inasema asilimia 20 ya juhudi huwa inazalisha asilimia 80 ya matokeo.
Yaani katika mambo kumi unayofanya, asilimia mbili tu ndiyo inazalisha asilimia 80 ya matokeo.
Kama unafanya kazi kwa masaa kumi kwa siku,masaa mawili pekee ndiyo yanayozalisha asilimia 80 ya matokeo unayoyapata.
Hiyo ina maana kwamba ukiyajua masaa mawili yenye manufaa makubwa na kuyazingatia hayo, kipato kitapungua kidogo, lakini utakuwa na muda mwingi zaidi, ambao unaweza kuutumia kufanya mengine muhimu na ukaingiza kipato kwa njia nyingine.
Chukua hatua; rafiki kokotoa muda wako wa kazi na uone ni masaa mangapi unayafanya kazi ambayo yanakupa matokeo mazuri unayoyataka.
Kisha masaa zingine ya ziada unaweza ukatumia kufanya kazi zingine muhimu na ukaingiza kipato kwa njia nyingine.
Mwandishi wako,
Maureen Kemei.
kemeimaureen7@gmail.com.