Matatizo 2 Makubwa Ya Fedha.

Rafiki yangu mpendwa sina uhakika kama itakufaa, lakini pale fedha inapotawala, matatizo mawili hujitokeza.

Tatizo la kwanza ni kuyeyusha misingi muhimu. Pale fedha inapokuwa kitu kikuu, watu hawaoni tena umuhimu wa kujenga misingi muhimu, badala yake wanaangalia kile kinachoingiza fedha kwa sasa.

Matokeo yake ni jamii inakosa taasisi muhimu zinazoweza kudumu kwa muda mrefu.

Chukua mfano kwenye biashara, pale ambapo lengo la biashara ni kuingiza faida kubwa kwa muda, hauwezi kufanya uwekezaji wa muda mrefu.

Matokeo yake ni biashara kushindwa kudumu kwa muda mrefu.

Tatizo la pili ni kuondoa utofauti na upekee. Pale fedha inapokuwa ndiyo lengo kuu, kila biashara inakazana inapunguza gharama ili kuongeza faida zaidi. Kinachotokea ni bidhaa na huduma kuwa na ubora wa hali ya chini na zinazofanana kote.

Hakuna aliye tayari kuingia gharama kuuza bidhaa au huduma ya kipekee, kwa sababu iyo hauwezi leta faida kubwa.

Hii imepelekea biashara nyingi ndogo kushindwa kushindana na biashara kubwa, kwa sababu biashara kubwa zina nguvu kubwa ya mtaji.

Biashara hizo ndogo zinaposhindwa na kufa, ule upekee unapotea kabisa. Na kinachobaki ni bidhaa na huduma zinazofanana kwa kila namna.

Haya yanachangia sana watu kushindwa kujitoa kwenye kitu kimoja kwa muda mrefu.

Fedha unapokuwa muhimu kuliko kingine chochote, ndiyo inayopewa kipaumbele kikubwa.

Rafiki yako,

Maureen Kemei.

kemeimaureen7@gmail.com

By Maureen Kemei

Author, psychologist.

Leave a comment

Your email address will not be published. Required fields are marked *