Namna Ya Kukamilisha To Do List Yangu.

Rafiki yangu mpendwa ni changamoto ipi umekuwa unakutana nazo kwenye kupangilia siku yako vyema.

Leo tunajifunza njia nzuri ya kuipangilia siku yetu vyema. Mambo hayo ni kama yafuatayo;

  1. Anza siku yako kwa kutafakari. Unapoamka asubuhi jiambie leo unaenda kukutana na watu watakaokuzingua, watakaokuangusha.
  2. Weka lengo la siku. Weka jambo moja na ulikamilishe ili kuwa na siku yenye mafanikio. Kufanya kitu kimoja kwa ustadi ni bora kuliko kufukuzana na mambo mengi.
  3. Kuweka vipaumbele. Peleka nguvu zako kwenye mambo ambayo unaweza kuyazithibiti, na mengine achana nayo.
  4. Jitahidi kukamilisha kazi muhimu mapema. Usijaribu kutoroka majukumu, pangilia yaliyo muhimu na msingi zaidi kabla hujavurukwa na mambo mengi. Kila maamuzi unayofanya yanatumia nguvu ya akili. ‘Eat that frog ‘
  5. Jifunze kila siku. Mazoezi ya mwili ni kujifunza. Kujifunza unaokoa muda na una onaongeza ufanisi kwenye kitu hicho unachojifunza.
  6. Weka muda wa kukamilisha vitu vya kawaida. Tenga muda wa usumbufu. Fanya kilicho muhimu yanayobaki ni ya ziada tu.
  7. Jioni tafakari siku yako mzima. Kama kipi nimefanya vizuri Leo? Kipi nimefanya vibaya leo? Vipi ni vitu vya kuboresha leo?.
  8. Kubali mambo yasiyoweza kubadilika. Huwezi kubadilisha upepo lakini unaweza kubadilika wewe ili kuendana na hayo.
  9. Fanya vitu kwa NIDHAMU kali sana. Kuna muda wa kukubali kila kitu na kuna wakati wakukataa vitu vyote. Kadiri unavyokataa vitu vizuri ndivyo unavyoruhusu kitu kilicho bora zaidi like. Nidhamu ndiyo funguo ya uhuru.
  10. Soma vitabu kwa ajili ya maendeleo ya kila siku. Jifunze kitu ambacho utakifanyia kazi moja kwa moja.

Rafiki kwa kuzingatia mambo haya utaweza kuishi siku yako kwa mafanikio zaidi. Tabia ya kitajiri ni kuwa bora zaidi.

Rafiki yako,

Maureen Kemei.

By Maureen Kemei

Author, psychologist.

Leave a comment

Your email address will not be published. Required fields are marked *