Ushauri Ambao Ningependa Kuwaambia Watoto Au Mtu Yeyote Ili Kuwa Na Maisha Bora Yenye Mafanikio Na Anthony Pompliano Kwenye Kitabu Chake Cha ( How To Live An Extraordinary Life).

Rafiki yangu mpendwa Anthony aliandikia watoto wake barua, huku anajishauri yeye mwenyewe kuhusu maisha aliyoyapitia.

Mahali alipopotia yeye aliandika barua 65. Karibu sana tujifunze.

  1. (How you do anything is how you do everything). Kwa mfano mchelewaji ndiyo asili yake, itakuathiri wewe iwe kazi ya mtu au kazi yako.
  2. (Today is a practical of tomorrow). Mafanikio siyo ajali. Tabia za kila siku kidogo kidogo ndiyo mchakato wako wa mafanikio.
  3. Yachonge kwenye jiwe maadili yako, maoni ya watu yaandike kwenye mchanga. Usiivunje maadili yako ya uaminifu.
  4. Smartest people read books 📚. Hautafanikiwa kwa kitu unacholazimishwa kufanya, bali utafanikiwa kwa kulazimishwa kuacha kufanya kwa mfano unapozuiwa kusoma unafaulu.
  5. Kukubali unapokosea. Makosa ni sehemu ya kujifunza. Kwa kukubali kuwa umekosea unajipa fursa mpya ya kufanya tena na kusonga mbele.
  6. Ubora hauna saa. Warren Buffett alianza kuwekeza akiwa na miaka 11, alianza kuwa billionea akiwa na miaka 40. Ukiharakisha mambo unaishia kupoteza.
  7. (Do it right do it light). Watu wanafanya kwa usahihi, linarahisisha mfumo.
  8. (Build things). Ili kuwa na maisha bora lazima kuna kitu unakijenga. Kwa mfano jenga biashara ilete matokeo makubwa, jenga huduma, jitoe ili kitu kiishi miaka mingi baada ya wewe kupita.
  9. (Action). Ukijifunza kitu chochote, chukua hatua.
  10. Maliza kitu ulichoanza. Mafanikio inachukua zaidi ya miaka kumi kwa mtu kufanya kitu na kufanikiwa, jipime mwenyewe.
  11. (Luck is not real). Tunatengeneza bahati zetu wenyewe. Kwenye maisha mambo yanaweza kutafsiriwa kwa uzuri au ubaya. Kwa mfano mtu kufukuzwa kazi na baadaye kupata kazi nyingine nzuri zaidi au kufanikiwa kwenye biashara.
  12. (Write two pages a day). Ndani ya mwaka mtu ana kitabu, andika jukumu moja kwa siku hatimaye unapata mwendo.
  13. Usijilinganishe na walio chini yako, bali jilinganishe na walio juu yako kimafanikio.
  14. Jenga sifa yako. Kwenye kitu ambacho hakiwezi kupotea. Vitabeba jina lako. Tambulika kwa sifa zako mwenyewe sio cheo chako.
  15. Uzoefu wa miaka mbili mara tano au uzoefu wa mwaka moja mara kumi. (Learning curve) Hujifunzi kitu kipya kila wakati. Lazima kila wakati uendelee kuwa bora zaidi, usiwe mzoefu ambaye husogei.

Chukua hatua, rafiki yangu mpendwa huu ndio ushauri ambao tunapaswa kufanyia kazi sisi wenyewe kwanza kabla ya kuwashuri watoto wetu au watu wengine. Mimi naifanyia kazi sasa hivi.

Rafiki yako,

Maureen Kemei.

By Maureen Kemei

Author, psychologist.

Leave a comment

Your email address will not be published. Required fields are marked *