Rafiki yangu mpendwa moja ya nguvu muhimu unayopaswa kuwa nayo maishani ni uwezo wa kuwaachia watu waendelee na safari yao—hasa wale wasioona thamani yako.
Kama utaendelea kushikilia mahusiano na watu wanaokudharau au kukufanya ujione mdogo, utapoteza kujiamini na hatimaye utaishi kwa mashaka na hofu.
Leo amua kujiamini! Jipende na jithamini kwa sababu thamani yako haiamuliwi na mtazamo wa wengine.
Usiruhusu maoni ya watu yakutawale au yakuzuie kufanikisha malengo yako.
Kila mtu ana safari yake ya maisha, na safari yako ni ya kipekee—hakuna anayepaswa kukufanya ujihisi huna maana.
Jiamini, jithamini, songa mbele! Muda wako ni wa thamani, tumia kwa ajili ya maendeleo yako na wale wanaokuthamini kweli.
Chukua hatua; rafiki kuanzia leo amini kwenye kujiamini,kijithamini na kujipenda. Achana na watu wanaonakuona kama huwezi chochote au hufai kwa lolote.
Na njia bora ya kujipenda ambayo nimejifunza kutoka kwa Kocha wangu Dr Makitrita Amani, ni kuweka akiba na uwekezaji. Njia bora ya kujilipa mwenyewe, kwa kufanya hivyo unatengeza kesho yako yenye matumaini kwako na wapendwa wako
Rafiki yako,
Maureen Kemei.